Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa
kituo cha Redio cha EFM, Denis Ssebo (kushoto), akizungumza katika
mkutano na waandishi wa habri Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu
kuendelea kufanyika kwa Tamasha la Muziki Bar kwa Bar baada ya
kumalizika kwa tamasha hilo kwa awamu ya kwanza. Kulia ni Mtangazaji,
Dina Marios.Na Dotto Mwaibale
KITUO cha Redio cha EFM kimeamua kuendelea kufanya tamasha la
muziki Bar kwa Bar baada ya kumalizika kwa tamasha hilo kwa awamu ya
kwanza.
Hayo yalibainishwa na Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa kituo hicho,
Denis Ssebo wakati akizungumza na waandishi wa habri Dar es Salaam leo
asubuhi kuhusu tamasha hilo.
"Baada ya kumalizika kwa Tamasha la musiku mnene Bar kwa bar awamu
ya kwanza, na mashabiki kuomba Burudani hiyo iendelea tena Kituo chetu
cha Redio cha Efm kimekubali ombi hilo na sasa tamasha hilo linarudi
tena kwa kishindo likiwa limeboreshwa kwakuongeza wigo wa kuwafikia
watu wengi zaidi" alisema Ssebo.
Alisema Muziki mnene bar kwa bar awamu hii bila kuwasahamu
wasikilizaji na mashabiki wa EFM katika wilaya za Kinondoni, Temeke na
Ilala kwa umuhimu wake na Wilaya mpya katika mkoa wa Dar es salaam,
Muziki mnene sasa utapelekwa pia katika mkoa wa Pwani.
Ssebo alitaja maeneo ambayo wanatakiwa kukaa tayari kwa Muziki
mnene bar kwa bar utakaoporomoshwa na Madjs wakali wa Efm, ni pamoja na
Kibaha, Mlandizi, Mkuranga, Bagamoyo, Kisarawe, Kigamboni na maeneo
mengine mengi kwa ajili ya kuhakikisha tunakonga nyoyo za mashabiki
wetu.
Alisema Muziki Mnene bar kwa bar mwaka huu inatarajiwa kuanza rasmi
Septemba 5 mwaka huu lakini katika kuelekea huko efm imeanza na muziki
mnene bango katika sehemu yako ya biashara ambako bwana E anapita na
ukiwa umeweka bango la EFM na unasikiliza matangazo yetu basi utapata
kifurushi chenye zawadi kibao.
Aliongeza kuwa mwishoni kutakuwa na Tamasha kubwa la hitimisho
ambalo litafanyika jijini Dar es salaam ambalo safari hii limeboreshwa
na kuongezwa vionjo vingi sana.
“Ninawaomba wasikilizaji wetu wakae mkao wa kula maana tutawafikia
na kuwamiminia Burudani ambayo pia itarushwa live kutoka eneo husika
kupitia kituo chao cha 93.7 EFM. Njoo tuonane, tufahamiane na tuijenge
Radio yetu efm ambayo kwetu Muziki unaongea”. alisema Ssebo.
Ssebo alipenda kutumia fursa hiyo kuwajulisha umma kwamba katika
kuhakikisha wanaendelea kutoa burudani iliyobora zaidi kupitia vipindi
vyao mbalimbali,sanjari na kuwa na watangazaji wenye ushawishi na uwezo
mkubwa wame mtambulisha kwenu mtangazaji Dina Marios ambaye wengi uwezo
wake mnaujua na sasa ameungana na wenzake wenye uwezo mkubwa katika
familia ya Efm.
No comments:
Post a Comment