Nay Wa Mitego afunguka uhusiano wake na Shamsa Ford
Staa wa Bongo Fleva,Elibarik Emmanuel ‘Nay Wa Mitego’amefunguka
uhusiano wake na mwigizaji wa filamu za Kibongo,Shamsa Ford baada ya
picha kadhaa kuzagaa mtandaoni wakiwa kimahaba wakipigana mabusu.Akipiga
Stori na TONYTZ.BLOG alisema kuwa hana uhusiano wa kimapenzi na mwanamke
yoyote kwa sasa siyo tu Shamsa Ford, na nafasi ipo kwa yoyote
anatakayekubali kuwa mpenzi wake.
‘’Jamani nipo singo kwa sasa sina uhusino na mwanamke yoyote na Shamsa
siyo mpenzi wangu,’’alisema Nay. Akizungumzia picha zilizozagaa
mtandaoni akipigana mabusu na mwigizaji huyo alisema kuwa hiyo ni filamu
yao mpya ya kimapenzi ambayo itatoka muda si mrefu kuanzia sasa.
‘’Ile picha ni vipande vya movie yetu ya kimapenzi mimi na Shamsa bado
hatujaipatia jina kwa sasa mashabiki wasubiri tu wataiona halafu Shamsa
hawezi kuwa mpenzi wangu kwa sababu ni ndugu yangu ni binamu
yangu,’’alisema Nay.
Shamsa naye alipoulizwa kuhusiano na picha hizo alisema ni filamu yao mpya wanafanya.
No comments:
Post a Comment