Akiongea
na East Africa Radio Ditto amesema kuwa alipigiwa simu na Chid Benz
aende studio ya Dhabu Records na alipokwenda alikutana na mdundo wa
wimbo wa 'Dar es Salaam Stand Up' ndipo alipopata mzuka wa kufanya
Chorus kali ya wimbo huo ambao ulipokelewa vizuri sana na mashabiki na
kuwa wimbo mkubwa.
"Nilikuwa nipo kimya muda mrefu sana, ghafla nikaona simu ya Chid
akaniita studio na nilipofika nilipewa mdundo uliokuwa mkali sana jambo
ambalo lilinifanya nipatwe na mizuka ya kufanya kazi ile kwa muda mfupi,
na kupitia wimbo ule ndipo safari yangu ya kwenye muziki ilifufuka
tena," alisema Lameck Ditto.
Ameongeza kuwa anakumbuka kabisa wimbo wa 'Dar es Salaam Stand Up' ulikuwa wimbo wake wa pili kufanya na msanii mkubwa nchini. Msanii Ditto kwa sasa ameegemea zaidi katika masuala ya kilimo japo hata sanaa anafanya lakini kwa sasa nguvu yake kubwa ameielekeza katika kilimo.
Ameongeza kuwa anakumbuka kabisa wimbo wa 'Dar es Salaam Stand Up' ulikuwa wimbo wake wa pili kufanya na msanii mkubwa nchini. Msanii Ditto kwa sasa ameegemea zaidi katika masuala ya kilimo japo hata sanaa anafanya lakini kwa sasa nguvu yake kubwa ameielekeza katika kilimo.
No comments:
Post a Comment