Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
Agizo hilo lilitolewa juzi na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro
Nyalandu (pichani), kwenye kikao cha wenyeviti wa vijiji hivyo na wadau
wa maliasili na utalii kilichofanyika kwa lengo la kujadili mgogoro
huo.
Nyalandu aliwataka Wanambomipa kuzungumza na wawekezaji na kupitia
mikataba baina yao huku akisisitiza kuwa serikali haitakubali iendelee
kutumika endapo itabainika kuwa na dosari.
Nyalandu aliyeongozana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya
Makazi, Willium Lukuvi na Waziri kivuli wa Maliasili na Utalii ambaye
pia ni Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa na
viongozi wengine alisema:
“Nimejaribu kuangalia mgogoro huu nimeona hisia zenu na nimegundua
na inabidi serikali ihakikishe kila mtu anapata haki yake," alisema na
kuongeza kuwa:
"Nilichogundua kuna wananchi ambao wamekosa fedha zao kutoka kwa
mwekezaji ambazo hazijalipwa muda mrefu, kuna rasilimali za kwenu ambazo
hamjazifaidi na badala yake wanafaidi wengine. ”
Vilevile aliagiza mkataba na mwekezaji yoyote Duniani anayetaka
kuwekeza vitalu vya uwindaji nchini ni lazima ipitiwe na serikali kabla
ya kusainiwa na mwekezaji huyo ili kujiridhisha haiwanyonyi wananchi kwa
manufaa ya wachache.
“Mikataba lazima niione kupitia wanasheria wangu wizarani,
tuipitishe na kama tunaona mkataba una matatizo tutaurudisha na
kuwaambia vipengele hivi vinawanyonya wananchi na hivyo vibadilisheni,”
alisisitiza Nyalandu
Awali alisema mgogoro huo unatokana na Mbomipa kudhani kuna uonevu
uliotokana na mikataba ilivyofanyika, Mbomipa kulaumu halmashauri kuu
ama mfumo wa uendeshaji ambao ndiyo uliowafikisha hapo.
Hata hivyo, aliwataka wanajumiya hiyo kuhakikisha kukutana na
kupitia upya mifumo ya utawala ili baadaye iwe mfano wa kuigwa na
jumuiya nyingine kama hiyo nchini.
Kwa upande mwingine, aliwashauri Mbomipa kukutaka na mwekezaji
anayedaiwa kuwa chanzo cha mgogoro huo kukubalina kuiondoa kesi yao
mahakamani.
" Hii ndiyo njia yangu yakuweza kuwasaidia ili mgogoro huu uweze
kumalizika kwa sababu taarifa niliyoipata mwekezaji alikubali kukaa na
Wambomipa," alisema.
Kwa upande wake, Waziri Lukuvi, alionyesha kushangazwa na mwekezaji huyo kukaidi zuio la mahakama kwa kuendelea kuwinda wanyama.
Vilevile alimhoji Waziri Nyalandu sababu za wizara yake kuendelea kutoa kibari cha uwindaji bila kutoa fedha kwa wanavijiji hao.
Lukuvi alisema wamemuita Waziri Nyalandu kwa lengo la kumaliza
mgogoro huo na wanavijiji hao, hivyo walipwe fedha zinazolingana na kile
kinachowindwa.
Mbomipa imeingia katika mgogoro huo baada ya kumtuhumu mwenyekiti
wao, Phillip Mkubata kushindwa kuendesha jumuiya hiyo kwa kuzingatia
katiba, kanuni, taratibu na kushindwa kuitisha mikutano ya kikatiba kwa
miaka miwili.
Tuhuma nyingine ni kubadili matumizi ya moja ya eneo la uwekezaji
la jumuiya hiyo lililotengwa kwa ujenzi wa kambi na hoteli za kitalii
na kuwa la uwindaji wanyamapori bila ridhaa ya mkutano mkuu wao.
Eneo hilo la kanda ya uwekezaji ya Lunda sehemu yake ya kilomita
mbili za mraba, lilitolewa kwa kampuni ya uwindaji kwa ajili ya ujenzi
wa kambi na hoteli za kitalii bila kutangazwa ili kuruhusu ushindani
kama sheria ya wanyamapori ya mwaka 2009 inavyotaka.
Wanajumuiya hao waliendelea kumtuhumu mwenyekiti huyo kwa
kushindwa kusimamia makusanyo na kutoa gawio kwa vijiji kila mwaka huku
akishindwa kukusanya mapato ya zaidi ya Sh. milioni 200 kwa kampuni
hiyo ambayo ilikabidhiwa eneo kwa zaidi ya miaka 10.
No comments:
Post a Comment