Syria yaonya dhidi ya shambulizi

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry alisema kuwa Marekani ilitumia kemikali aina ya Sarin kushambulia wananchi

Hatua yoyote ya kijeshi itakayochukuliwa na Marekani dhidi ya Syria, huenda ikachochea usaidizi kwa wapiganaji waal-Qaeda na washirika wake kwa mujibu wa taarifa kutoka Damascus.
Naibu waziri wa mambo ya nje wa Syria, Faisal Mekdad pia aliambia BBC kuwa makundi ya wapiganaji waliojihami, yalitumia silaha za kemikali wala sio wanajeshi wa Syria.

Marekani awali ilisema kuwa ilikuwa na ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa serikali ya Assad ilitumia kemikali aina ya Sarin katika shambulizi baya sana wiki jana .
Rais Barack Obama ameahidi kuchukua hatua kali dhidi ya Syria lakini mwanzo anataka baraza la Senate kupigia kura hoja hiyo kabla ya kuchukua hatua zozote dhidi ya Syria.
Wabunge wa Marekani wanatarajiwa kukutana na maafisa wa ikulu ya White House huku maafisa hao wakiwa na imani kuwa wataunga mkono hoja ya Obama.
Hata hivyo hatua ya Obama mwanzo kutaka baraza la Senate kuunga mkono hatua ya serikali kutaka kushambulia Syria imewashangaza wengi hasa washauri wake wa karibu.
Sio wazi kuwa Obama ataungwa mkono hasa na wabunge wa bunge la waakilishi ambao wengi ni wa chama cha Republican.
Labda Pia kwenye Senate huenda asipate kuungwa mkono. Bila shaka hii itakuwa kura yenye wasiwasi kwa Obama.
Ikiwa Congress haitaunga mkono hoja ya Obama basi huenda, likawa jambo baya sana kwa utawala wake.
Tayari kamapeini imeanzishwa ya kuwashawishi watu nchini Marekani kuwa ni jambo jema kwa serikali ya Obama kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Syria.
Lakini kwa kukosa kuchukua hatua za mashambulizi na badala yake kuomba idhini ya baraza la Senate itakuwa mchezo wa pata potea kwa Obama.

No comments:

Post a Comment