MAZOEZI YAURUDISHA MWILI WA STRA WA FILAMU TZ RAY.

 
KWA wale waliokuwa wakichongachonga wanayoyajua wenyewe, watakuwa wameumbuka sababu staa wa sinema za kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameanza kupata mwili kama zamani.

Kudhihirisha kama mwili wake umeanza kurudi kama zamani, paparazi wetu alimnasa staa huyo katika uzinduzi wa video ya wimbo wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, My Number One uliofanyika katika Hoteli ya Serena, Posta jijini Dar na kuona mwili wa staa huyo ulivyojengeka upya.
“Mazoezi ndiyo kila kitu katika mwili wangu, hayo wanayoyasema watasema lakini mimi ni msanii najua namna ya kuutengeneza mwili wangu kadiri ninavyotaka,” alisema Ray.

No comments:

Post a Comment