Moyes aanza kazi kwa ushindi.
Kocha wa Manchester United David Moyes hii leo ameanza rasmi kibarua
chake kama kocha wa timu hiyo kwenye mechi ya ushindani baada ya
kuiongoza timu hiyo kupata ushindi wa wa mabao mawili kwa bila katika
mchezo wa kuwania ngao ya jamii dhidi ya Wigan Athletic .
United ilifunga mabao yake kupitia kwa mfungaji bora wa ligi kuu ya
England kwa msimu uliopita Robon Van Persie ambaye alifunga mabao yote
mawili .
United iliingia kwenye mchezo huo bila mshambuliaji wake Wayne Rooney
ambaye hakuchaguliwa kwa kuwa ni majeruhi huku mustakabali wake ndani
ya klabu hiyo ukibakia kuwa kitendawili .
Beki wa Manchester United ambaye pia ni nahodha msaidizi wa timu hiyo
Mfaransa Patrice Evra alikuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya
kucheza kwa kiwango cha juu ambapo alichangia kwenye ufungaji wa mabao
yote mawili.
Taji la Ngao ya Jamii linakuwa taji la kwanza kwa kocha mpya David
Moyes tangu alipoteuliwa kurithi nafasi ya kocha wa zamani Sir Alex
Ferguson mwishoni mwa msimu wa ligi ulioisha .
David Moyes ataanza rasmi kampeni ya utetezi wa ubingwa wa ligi kuu
ya England kwa klabu yake wiki ijayo wakati Manchester United
watakapovaana na Swansea City kwenye mhezo wao wa kwanza wa ligi .
Story Za Michezo Kwa Hisani Ya Benki Ya NMB.
No comments:
Post a Comment