Aliyekuwa mgombea Ubunge kupitia Chama Cha ACT Wazalendo jimbo la Kinondoni, Kalama Masoud 'Kalapina' (kulia) akizungumza na wanahabari, kushoto kwake ni Afisa Habari wa ACT Wazelendo, Khamis Abdallah.
Kalapina akionesha msisitizo wa jambo wakati akiongea na wanahabari (hawapo pichani).
Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.
ALIYEKUWA mgombea Mbunge
katika Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Kalama
Masoud ‘Kalapina’ ameibuka na kupinga matokeo akidai atakwenda
mahakamani.
Akizungumza na wanahabari leo Makao Makuu
ya chama hicho Kijitonyama jijini Dar es Salaam, Kalapina amesema
matokeo yaliyompa ushindi mgombea wa chama cha wananchi CUF ambaye
alikuwa anaungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi
UKAWA, Abdul Mtulia yalikuwa yamesheheni dosari kubwa.
Amesema katika kata 19 zilizopo katika Jimbo la Kinondoni, mawakala
wake walitishiwa na kulazimika kuacha kusimamia vituo walivyokuwa
wamepangiwa.Kalapina alitaja baadhi ya maeneo aliyodai mawakala wake
walitishiwa na baadae kuamua kuondoka kuwa ni kata za
kijitonyama,Tandale, Ndugumbi pamoja na Kigogo.Alieleza kuwa baada ya kubaini matatizo yote hayo alilazimika kugomea kusaini karatasi ya wagombea ubunge, akiongeza kuwa hatua iliyobaki kwa sasa ni kwenda kufungua kesi mahakamani.“Natarajia kwenda mahakamani kutaka haki, kwa hiyo Jumatatu au Jumanne ijayo nakwenda kufungua kesi,” alisema kalapina.
No comments:
Post a Comment