Kundi la waislamu lahukumiwa miaka 22 jela


Mahakama moja nchini Ethioipia imelipiga hukumu ya miaka 22 jela kundi moja la waislamu chini ya sheria tata ya kukabiliana na ugaidi.
Washukiwa hao 18 walishtakiwa mwezi uliopita kwa mashtaka ikiwemo lile la ugaidi na njama ya kubuni taifa la kiislamu.
Walikamatwa miaka mitatu wakati wa maandamano ya kupinga serikali kuingilia maswala ya kidini.
Walikana mashtaka hayo na kulalama kwamba walinyanyaswa wakati walipokuwa kizuizini.
Wakati wa ziara ya rais Obama nchini humo baadhi ya wanaharakati walimueleza kuhusu kesi hiyo.

No comments:

Post a Comment