KUTANGAZA BIASHARA NASISI AU KUTUMA VIDEO NA AUDIO 0684 524265
Ebola:Shule zafunguliwa Sierra Leone
Shule
ambazo zimekuwa zimefungwa nchini Sierra Leone tangu mwezi Julai mwaka
uliopita kutokana na mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola zitafungwa hii
leo jumanne.
Mataifa mengine yalioathirika na mlipuko huo wa Ebola
Magharibi mwa Afrika Guniea na Liberia yaliruhusu kufunguliwa kwa
shule zao mwanzoni mwa mwaka huu. Shirika la afya duniani WHO limesema kuwa Ebola bado imebaki kuwa janga la kimataifa.
WHO inasema kuwa ugonjwa wa Ebola uliwaua karibu watu 10,600
Takwimu za hivi majuzi
zinaonyesha kuwa kuwa ni visa vipya 30 vya ugonjwa wa Ebola
vilivyothibitishwa nchini Guinea na Sierra Leone ikilinganishwa na mamia
ya visa hivyo siku za nyuma. WHO inasema kuwa ugonjwa wa Ebola uliwaua karibu watu 10,600 katika mataifa hayo ya Magharibi mwa Afrika. Aidha WHO inasema kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kuweka tahadhari kuu dhidi ya mlipuko huu ama mwengine wa Ebola.
No comments:
Post a Comment