Bunge la Tanzania linaanza vikao vyake
wiki ijayo, moja ya ishu ambayo wanasiasa na wanaharakati mbalimbali
wamekuwa wakishinikiza kufanyiwa maamuzi ni ishu ya Escrow, mwezi
DECEMBER, 2014 Rais Kikwete alitangaza kumsimamisha kazi Waziri Anna Tibaijuka kutokana na ishu ya fedha za Escrow ambazo kulikuwa na utata kwamba ni za umma ama za IPTL.
Vuguvugu lililobaki likawa kuwawajibisha
Prof. Muhongo pamoja na Wenyeviti watatu wa Kamati za Bunge ambao
walitajwa pia kuingiziwa pesa hizo, leo Prof. Muhongo ameitisha kikao na
waandishi wa Habari ofisini kwake na kutangaza kujiuzulu nafasi ya
Uwaziri.
Anakuwa Waziri wa pili kujiuzulu huku
kukiwa na taarifa Magazetini leo kwamba Wenyeviti wa Kamati za Bunge nao
pia wameachia nafasi hizo ili wachaguliwe wengine kabla ya Bunge kuanza
Jumanne wiki ijayo.
endelea kufuatilia sakata hili kupitia tonytz.blog utafaham zaidi.
No comments:
Post a Comment