Kuhusu ishu ya Escrow, ikufikie hii taarifa ya Waziri Muhongo alichokitangaza leo.

Breaking News
Bunge la Tanzania linaanza vikao vyake wiki ijayo, moja ya ishu ambayo wanasiasa na wanaharakati mbalimbali wamekuwa wakishinikiza kufanyiwa maamuzi ni ishu ya Escrow, mwezi DECEMBER, 2014 Rais Kikwete alitangaza kumsimamisha kazi Waziri Anna Tibaijuka kutokana na ishu ya fedha za Escrow ambazo kulikuwa na utata kwamba ni za umma ama za IPTL.

Vuguvugu lililobaki likawa kuwawajibisha Prof. Muhongo pamoja na Wenyeviti watatu wa Kamati za Bunge ambao walitajwa pia kuingiziwa pesa hizo, leo Prof. Muhongo ameitisha kikao na waandishi wa Habari ofisini kwake na kutangaza kujiuzulu nafasi ya Uwaziri.
Anakuwa Waziri wa pili kujiuzulu huku kukiwa na taarifa Magazetini leo kwamba Wenyeviti wa Kamati za Bunge nao pia wameachia nafasi hizo ili wachaguliwe wengine kabla ya Bunge kuanza Jumanne wiki ijayo.
endelea kufuatilia sakata hili kupitia tonytz.blog utafaham zaidi.

No comments:

Post a Comment