Part II ya matokeo ya UEFA Champions League.


uefa uefa uefa
Michuano ya UEFA Champions League iliendelea hapo jana ikiwa kwenye sehemu yake ya pili ya mzunguko wa pili wa hatua ya makundi .
Mabingwa watetezi wa michuano hiyo Bayern Munich wakiwa ugenini kwenye uwanja wa Etihad hawakuwa na huruma na vijana wa Manuel Pelegrini Manchester City baada ya kuwafunga 3-1 .
Bayern wanaoongozwa na Pep Guardiola walifunga kupitia kwa Frank Ribery ,Arjen Robben na Thomas Mueller huku Alvaro Negredo akifunga bao la City .
uefa uefa
Timu nyingine toka England Manchester United ambayo ilikuwa ugenini huko Ukraine ilitoka sare na Shakhtar Donetsk  ambapo timu hizo zilifungana bao 1-1. United walianza kufunga kupitia kwa Danny Welbeck kabla ya kiungo Mbrazil Taison hajaisawazishia Shakhtar.
Mabingwa wa Ufaransa Paris St Germain wakiwa nyumbani kwao kwenye uwanja wa   Parc-De-Princess waliwafunga Benfica 3-0 . Wafungaji wa PSG walikuwa Zlatan Ibrahimovic ambaye alifunga mabao mawili na Marquinhos .
Nao Real Madrid waliwafunga Fc Copenhagen 4-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani Santiago Bernabeu . Cristiano Ronaldo na Angel De Maria walifunga mabao mawili kila mmoja kwenye mchezo huo.
uefa uefa uefa uefa
Katika michezo mingine Juventus na Galatsasaray walitoka sare ya 2-2 katika mchezo wa kwanza kwa Galatasaray tangu walipomuajiri kocha mpya Roberto Mancini , CSKA Moscow nao walishinda mchezo wao dhidi ya Viktoria Plzen kwa matokeo ya 3-2 , Bayer Leverkusen wakawafunga Real Sociedad 2-1  na Olympiakos wakaifunga Anderletch 3-0.
uefa didi uefa uefa
 Story Za Michezo Kwa Hisani Ya Benki Ya NMB.

No comments:

Post a Comment