Aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini
Nlson Mandela amemaliza siku moja nyumbani kwake Johansberg baadha ya
kuondoka hospitalini alikokuwa amelazwa kwa zaidi za miezi mitatu
akipokea matibabu kwa maambukizi ya mapafu anayougua.
Nelson Mandela kwa sasa anendelea kupata nafuu
nyumbani. Serikali ya Afrika Kusini imesema atakuwa akipata huduma sawa
za zile alizokuwa akipewa hospitalini jijini Pretoria.
Maafisa wa serikali wameongezea kuwa
nyumba yake imekarabatiwa kuwezesha madakatari kumtibu akiwa humo.
Madakatri wataalam ambao wamekuwa wakimshughulikia wataendela kumtibu
nyumbani mwake, lakini ikiwa hali yake ya afya itahitaji huduma za
hospitali basi atarejeshwa humo bila kuchelewa.
Inasemekana kurudi nyumbani kwa Mandela kumetia
matumaini kwa familia yake pamoja na taifa la Afrika Kusini. Hata hivyo
Mzee Mandela bado anaonekana mwenye afya dhaifu.
Serikali ya Afrika Kusini ilisema hapo jana kuwa Mandela, alitolewa hospitali ambako amekuwa akitibiwa mapafu tangu mwezi Juni.
Taarifa katika tovuti ya rais wa Afrika Kusini
ilieleza kuwa Bwana Mandela bado ni mahtuti na hali yake wakati mwengine
inabadilika.
Lakini madaktari wake wanaamini akiwa nyumbani kwake mjini Johannesburg atapata matibabu sawa na yale ya hospitali.
Serikali imesema inamtakia mema wakati akiendelea na matibabu.
No comments:
Post a Comment