DAKIKA
za lala salama za usajili wa majira ya kiangazi, hatimaye Manchester
United imemnasa Marouane Fellaini kutoka Everton kwa ada ya uhamisho
ya pauni milioni27.5.
Jaribio
la United kutaka kumsajili nyota wa Athletic Bilbao, kiungo Ander
Herrera liligonga mwamba baada ya timu hizo kushindwa kukubaliana dau la
pauni milioni 30.5 kama ada ya kumnunua.
Sasa
kocha wa Man United, David Moyes amekutana na kijana wake waliyekuwa
wote Everton na kiukweli amemfukuzia kwa muda mrefu mpaka dakika za lala
kwa buriani za usajili wa kiangazi barani Ulaya.
Kiungo
huyo wa Ubelgiji, Fellaini amekuwa akitakiwa kuungana na kocha wake wa
zamani, Moyes na hakuwa na chaguo zaidi, isipokuwa kutua United.
Fellaini
amepewa ruhusa ya kuchelewa kujiunga na kikosi chake cha timu yake ya
taifa, ili kukamilisha uhamisho wake mchezaji huyo mwenye umri wa miaka
25 kutua United, ambao ulikuwa unashughulikiwa na baba yake, Abdellatif.
United
ilituma ofa tofauti kwa wote Fellaini na Leighton Baines mapema majira
haya ya joto, ikianza na Pauni Milioni 28 jumla kwa wote na baadaye
Milioni 36, ambazo zote zilipigwa chini na Everton.
Na
inafahamika kwamba United ilijaribu kumsajili Mesut Ozil aliyetua
Arsenal kwa Pauni Milioni 42 kutoka Real Madrid na ilitoa ofa iliyodunda
na Pauni Milioni 34 kwa mchezaji mwingine wa Real, Sami Khedira kabla
ya kujaribu kwa nyota wengine wa klabu hiyo Luka Modric bila mafanikio.
Jembe jipya mjini: Fellaini akiwa amepozi na uzi wa Manchester United
Limewasili: Fellaini akiwasili na kocha wake Moyes maeneo ya Carrington
No comments:
Post a Comment