Baada
ya zaidi ya miaka 6 ya ukimya uliomuwezesha kumaliza degree yake pia
kwenye chuo cha Tumaini Dar es salaam, King Crazy GK wa East Coast leo
August 28 2013 amerudi rasmi kwenye muziki wa bongofleva na kusema hii
ni vita kwenye soka la muziki huu ambapo ameachia single yake mpya
inaitwa Baraka au laana ft Yuzo ambayo unaweza kuisikiliza hapa chini.Yako mengi aliyoyazungumza ambapo pia aliambatana na wakali wengine ambao walikuepo kitambo East Coast kama Ay na Mwana FA lakini pia mtu kama Pauline Zongo na wengine.
Yote aliyoyasema utayapata hapa kupitia video na pia nitaandika kilichosemwa ili kwa wale wasioweza kutazama video wasome… cha muhimu ni kuwa karibu na Millard Ayo facebook, twitter na instagram kwa jina hilohilo ili usipitwe na chochote na huko ndio kutakua kujiunga kwako kuwa mwanachama mtu wangu.








No comments:
Post a Comment