HONGERA YANGA KWA KUTWAA NGAO YA JAMII KWA KUWAPIGA AZAM FC RISASI 1-0… LAKINI JICHO LA TATU LIMEBAINI UBORA WA LUHENDE NA UGONJWA WA TAIFA WA UBUTU WA SAFU YA USHAMBULIAJI !!
Wakati
mashabiki wakifurika kwa wingi kwenda kuutazama mchezo wa ngao ya jamii
hapo jana baina ya mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara, klabu ya Yanga
dhidi ya Makamu bingwa, Wana Lambalamba Azam fc katika uwanja wa Taifa
jijini Dar es salaam, binafsi sikwenda kushangilia timu yoyote bali
nilienda kushuhudia mambo makubwa mawili.
Mechi
ya jana kwa upande wangu ilikuwa burudani kubwa sana kwani nilishuhudia
soka safi la ushindani, kwani timu zote “zimefundwa” kiukweli.
Maarifa
ya makocha wawili wa kizungu, Ernie Brandts kwa Yanga na Sterwart John
Hall wa Azam, yanaonekana kuwakolea vijana wa Kitanzania na nje ya
Tanzania wanaozichezea timu hizo mbili.
Ukihusianisha
majina ya “Yanga na Azam fc” hayana ushindani, na hii inatokana na
Yanga kuwa klabu kongwe zaidi hapa Tanzania na imejiimarisha kwa kuwa na
mashabiki lukuki zaidi ya Azam ambao ndio kwanza wameanza safari yao,
lakini kwa kuangalia aina ya mpira unaochezwa na timu hii yenye makazi
yake Chamazi, najiridhisha kuwa ni timu bora iliyojipanga na itafika
mbali.
Inafahamika
kuwa mechi ya jana hiyo ilimazika kwa Yanga kushinda kwa bao 1-0, bao
likifungwa na Salum Abdul Telela katika dakika ya pili tu, watoto wa
mjini huita “Dakika za Asubuhi”, kwangu mimi matokea hayana maana sana,
lakini nilijivuta kwenda uwanja wa Taifa kwa mambo mawili kama
nilivyosema hapo juu.
Kwanza,
nilienda kumuangalia bwana mdogo aliyeshutumiwa na mashabiki wengi wa
soka nchini kwa kusababisha penati na kuwa uchochoro wakati Taifa Stars
ilipofungwa na Uganda mabao 3-1 jijini Kampala kuwania kucheza fainali
za CHAN, huyu si mwingine bali ni kinda David Luhende.
Watu
walizungumza sana juu ya uwezo wake,wengine walisema kocha Kim alikosea
kumpanga mechi yake ya kwanza Taifa Stars dhidi ya Uganda, mechi kubwa
ya mashindano na alikuwa uchochoro, lakini wakasahau kuwa hata “Mbuyu
ulianza kama mchicha”. Binafsi nilijiridhisha kuwa atakuwa bora zaidi
kwa uwezo alioonesha kwa siku ya kwanza, licha ya kuwa na mapungufu.
Naupenda
sana msemo wa kocha wa klabu ya Mbeya City ya jijini Mbeya, Juma
Mwambusi, huwa anasema “Mchezaji yeyote mwenye uzoefu alianza kutokuwa
na uzoefu, akapewa nafasi akacheza na baadaye kupata uzoefu, hivyo
lazima wachezaji wote wapate nafasi ya kucheza ndipo wajenge uzoefu,
usipompa nafasi kijana atatoa wapi uzoefu”?.
Nina
uhakika hata kocha wa Stars, Kim Poulsen ana falsafa hiyo ya kuwaamini
wachezaji vijana na kuwapa majukumu mazito kama alivyofanya kwa David
Luhende ambaye aliitwa kwa mara ya kwanza Taifa stars mwezi uliopita na
kucheza mechi ngumu ya mashindano dhidi ya Uganda.
Ukitaja
jina la Luhende, wapenda michezo wengi waliokuwa na malengo ya kwenda
Afrika kusini kushuhudia fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa
wachezaji wa Ligi za ndani, CHAN nywele zinawasisimka kutokana na madudu
aliyofanya nyota huyo kinda baada ya kuitwa kuziba pengo la Shomary
Kapombe aliyekwenda Ulaya kujaribu bahati yake ya kucheza soka la
Mataifa.
Luhende
alikuwa uchochoro vibaya sana kwani alipitisha mipira mingi ya hatari
na kuunawa mpira katika eneo la hatari na mwamuzi kuwazawadia mkwaju wa
penati Uganda na kufunga bao la pili kupitia kwa nyota wao Brian Majwega
na kuwachanganya stars waliolala kwa mabao 3-1.
Jana
bila kuwa na roho ya kinyongo, bila kujali unazi wa timu, Luhende
alipiga mpira mkubwa sana na ilikuwa burudani kubwa wanapokutana na
Khamis Mcha “Vialli” wa Azam, ufundi mkubwa ulioneshwa na hii inaashiria
hatari kwa beki wa kushoto wa Yanga, Oscar Samwel Joshua.
No comments:
Post a Comment