25 WACHUKUA FOMU ZA UCHAGUZI TFF

25 WACHUKUA FOMU UCHAGUZI TFF
Wanamichezo
 25 wamechukua fomu kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi
 wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unaotarajiwa kufanyika 
Oktoba 27 mwaka huu.
Fomu
 hizo zilianza kutolewa juzi (Agosti 16 mwaka huu) ambapo wawili 
wamechukua nafasi ya Rais na wengine wawili Makamu wa Rais wakati 
waliobaki wanaomba ujumbe wa Kamati ya Utendaji wakiwakilisha kanda 
mbalimbali.
Waliochukua
 fomu za kuomba kuteuliwa kuwa wagombea urais ni Jamal Malinzi na Omari 
Musa Nkwarulo wakati umakamu wa rais hadi sasa umewavutia Wallace Karia 
na Ramadhan Nassib.
Waliochukua
 fomu za ujumbe ni Athuman Kambi, Charles Komba, Davis Mosha, Elias 
Mwanjala, Eliud Mvella, Epaphra Swai, Farid Nahdi, Hussein Mwamba, Jumbe
 Magati, Kamwanga Tambwe na Khalid Mohamed.
Wengine
 ni Muhsin Balhabou, Omari Abdulkadir, Omari Walii, Samwel Nyalla, 
Shaffih Dauda, Stanley Lugenge, Twahir Njoki, Vedastus Lufano, Venance 
Mwamoto na Wilfred Kidao. 
Kwa upande wa Bodi ya Ligi Kuu aliyechukua fomu mpaka sasa ni Hamad Yahya anayeomba kuteuliwa kugombea nafasi ya uenyekiti.
Fomu za maombi pia zinapatikana kupitia tovuti ya TFF ambayo ni www.tff.or.tz Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni saa 10 kamili jioni ya Agosti 20 mwaka huu.2
Fomu
 zikiambatanishwa na risiti ya malipo (receipt) au malipo ya benki 
(deposit slip) kupitia akaunti ya TFF namba 01J1019956700 iliyoko CRDB 
tawi la Holland House zirejeshwe kwa Katibu Mkuu wa TFF kwa mkono au kwa
 barua pepe (email) ambayo ni tanfootball@tff.or.tz .
MECHI YA NGAO YA JAMII YAINGIZA MIL 208
Mechi
 hiyo ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kuashiria ufunguzi wa msimu 
mpya wa 2013/2014 iliyochezwa jana (Agosti 17 mwaka huu) Uwanja wa 
Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 208,107,000. Washabiki 26,084 
walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo ilimalizika kwa Yanga 
kushinda Azam bao 1-0.
Mgawanyo
 wa mapato ya mechi hiyo uliokuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya
 Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 31,745,135.59, asilimia 10 ya mchango wa 
kusaidia jamii sh. 20,810,700, gharama ya tiketi sh. 7,309,866.
Uwanja
 sh. 22,236,194.76, gharama za mchezo sh. 13,341,716.86, Chama cha Mpira
 wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 5,188,445.44, TFF sh. 
13,341,716.86 na Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 
6,670,858.43. Kila klabu imepata mgawo wa sh. 43,731,183.03. 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
No comments:
Post a Comment