Home » Michezo » Jezi namba 11 ya Bale Real Madrid yaingia sokoni.

Jezi namba 11 ya Bale Real Madrid yaingia sokoni.

Gareth-Bale-2134739
Huku  wakiwa wanatajwa kuwa kwenye hatua za mwisho za kukamilisha usajili wake toka klabu ya Tottenham Hotspurs klabu ya Real Madrid imeanza kuziweka sokoni jezi zenye jina la mchezaji Gareth Bale .

Kwa muda mrefu Real wamekuwa kwenye mazungumzo na Spurs kuhusu usajili wa mchezaji huyu ambapo inaaminika kuwa Real wametenga dau ambalo litamfanya mchezaji huyo kuwa mchezaji ghali kuliko wote duniani na hakuna uficho kuwa rais wa Madrid Florentino Perez amekuwa akimsaka Bale kwa udi na uvumba kwa muda mrefu.
BALE KIT
Bale amekuwa mkimya muda wote ambapo hajalizungumzia suala hili huku taarifa za ndani zikisema kuwa ameshawaaga wachezaji wenzie wa Tottenham huku pia akiwaambia wachezaji wenzie kwenye kambi ya timu ya taifa ya Wales kuwa hatavaa jezi ya Spurs tena .
Jezi za Gareth Bale zenye namba 11 mgongoni zimeingia rasmi sokoni wiki hii nchini Hispania huku zikiwa tayari zimeshaanza kuuzwa mapema zaidi kwenye kisiwa cha Gibraltar.
Mtandao wa Real Madrid unaonyesha jina la Gareth Bale likiwa kwenye orodha ya jezi ambazo mashabiki wa klabu hiyo wanaweza kuagiza.
bale madrid
Inaaminika kuwa tayari makubaliano ya mauzo ya mchezaji huyo baina ya timu mbili na mchezaji mwenyewe yamekwishamalizika na mchezaji huyo atathibitishwa kuwa mchezaji wa Real siku si nyingi .

No comments:

Post a Comment