Magufuli apendekeza Daraja la Kigamboni lipewe jina la Nyerere.

Magufuli apendekeza Daraja la Kigamboni lipewe jina la Nyerere. 

Rais wa Tanzania John Magufuli amependekeza daraja mpya la Kigamboni lipewe jina la mwanzilishi wa taifa hilo Mwalimu Julius Nyerere.
Akiongea muda mfupi kabla ya kuzindua rasmi daraja linafaa kupewa jina la Mwalimu Julius Nyerere kutokana na mchango wake kwa nchi hiyo.
Daraja la Kigamboni lilianza kutumika tarehe 16 Aprili, 2016 na lina urefu wa mita 680 na barabara unganishi upande wa Kurasini na Kigamboni zenye urefu wa kilomita 2.5.

Ujenzi wake ulifanywa na kampuni ya China Railway 15 Group ikishirikiana na kampuni ya China Bridge Engineering Group.
Daraja hilo ndilo la kwanza la kubeba uzito wa barabara kwa kutumia nyaya Afrika Mashariki na la tatu Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara bila kuhesabu Afrika Kusini.
Linamilikiwa na serikali ya Tanzania na Hazina ya Malipo ya Uzeeni (NSSF) kwa 40% na 60% mtawalia na litachukua nafasi ya feri ya MV Magogoni.
Wenye magari na pikipiki watahitajika kulipa kutumia daraja hilo lakini wapitanjia watavuka bila malipo.Ujenzi wa daraja hilo, ambao uligharimu dola 128 milioni za Kimarekani, ulianza mwaka 2012.


No comments:

Post a Comment