Rais wa Tanzania John Magufuli
amependekeza daraja mpya la Kigamboni lipewe jina la mwanzilishi wa
taifa hilo Mwalimu Julius Nyerere.
Akiongea muda mfupi kabla ya kuzindua rasmi daraja linafaa kupewa
jina la Mwalimu Julius Nyerere kutokana na mchango wake kwa nchi hiyo.Daraja la Kigamboni lilianza kutumika tarehe 16 Aprili, 2016 na lina urefu wa mita 680 na barabara unganishi upande wa Kurasini na Kigamboni zenye urefu wa kilomita 2.5.
Daraja hilo ndilo la kwanza la kubeba uzito wa barabara kwa kutumia nyaya Afrika Mashariki na la tatu Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara bila kuhesabu Afrika Kusini.
Linamilikiwa na serikali ya Tanzania na Hazina ya Malipo ya Uzeeni (NSSF) kwa 40% na 60% mtawalia na litachukua nafasi ya feri ya MV Magogoni.
No comments:
Post a Comment