MAHAKAMA YAMFILISI WEMA


YAMETIMIA! Ni kweli hakuna marefu yasiyokuwa na ncha! Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu aliyesifika kwa kumwaga fedha kila kukicha  ameanza  kufilisiwa, Ijumaa Wikienda lina habari ya kipekee kuhusu mrembo huyo.

Wema Isaac Sepetu.
MAHAKAMA YAANZA
Achilia mbali watu binafsi wanaochukua vyao baada ya mambo kuzidi kumwendea ndivyo sivyo, habari ya uhakika ni kwamba Mahakama ya Ilala, Dar imeridhia kukamatwa kwa lile gari lake la kifahari aina ya Audi Q-7 lenye namba za usajili T 973 BUJ lililokuwa likiwakosesha akina dada usingizi na kukabidhiwa kwa mmiliki halali kwa kuwa Wema alikuwa nalo kimagumashi.


Gari aina ya Audi Q-7 lenye namba za usajili T 973 BUJ alilokuwa akiendesha Wema.
Kwa mujibu wa vyanzo vilivyoenda shule vya Ijumaa Wikienda, gari hilo lilikamatwa Januari 2, mwaka huu Namanga, Oysterbay jijini Dar likiwa mikononi mwa kijana wa kiume aliyedaiwa kuwa ni mdogo wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’.
“Alikuwa nalo yule dogo ‘waiti’, mdogo wake huyu msanii Diamond. Alikuwa na wenzake pale Namanga kuna kibarabara cha vumbi, walikuwa wanarekodi video. Jamaa walikuwa wanalifuatilia so lilipopaki ndipo wakalipiga ‘tanchi’ (kulikamata),” kilisema chanzo chetu cha kuaminika.
Gari hilo baada ya kukamatwa.
Ilifahamika kuwa gari hilo lilikamatwa na kampuni kiboko ya madalali wa mahakama nchini (court brokers) ya jijini Dar iitwayo Unyangala Auction Mart Ltd & Court Brokers yenye ofisi zake kwenye Jengo la Harbour View Tower ‘JM-Mall’, Dar.
WEMA ACHANGANYIKIWA
Habari za uhakika zilidai kuwa kabla ya kulipeleka ‘yadi’ dogo huyo aliyekamatwa na gari hilo aliwasiliana na Wema na kumjulisha ambapo ilisemekana kwamba bidada huyo alichanganyikiwa.
Baada ya pale walilipeleka gari hilo kwenye yadi yao hiyo kisha kuwasiliana na mmiliki halali tayari kwa kumkabidhi.

Gari hilo likikabidhiwa kwa mmiliki halali.

No comments:

Post a Comment